Posts

WATUMISHI NGORONGORO KUNUFAIKA NA MILIONI 500, WAONYWA MIKOPO KAUSHA DAMU.

Image
  NGORONGORO.  Halmashauri ya Wilaya ya Ngorongoro imetenga Sh milioni 500 kwa ajili ya watumishi wa umma, ikiwa ni sehemu ya mpango wa kuwainua kiuchumi watumishi wa kada zote. Akikabidhi mikopo hiyo, Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo, Murtallah Sadick Mbilu, amesema lengo la mpango huo ni kuwasaidia watumishi kujikwamua na changamoto za kifedha na kuboresha maisha yao. Amesema mikopo hiyo pia inalenga kupunguza utegemezi wa mikopo isiyo rasmi yenye riba kubwa maarufu kama kausha damu. Mbilu amewataka watumishi kutumia mikopo hiyo kwa malengo yaliyokusudiwa ili iwe na tija kwao binafsi na katika utekelezaji wa majukumu yao ya kazi. Aidha, amesisitiza kuwa utoaji wa mikopo hiyo utafanyika kupitia mfumo rasmi wa watumishi ili kuhakikisha uwazi, usawa na kuepusha mgongano wa maslahi. Ameongeza kuwa utekelezaji mzuri wa mpango huo utachangia kuongeza ufanisi wa watumishi na kuboresha utoaji wa huduma kwa wananchi.

WANANCHI WA NGORONGORO WAIBUA WASIWASI KUHUSU MAPENDEKEZO YA TUME.

Image
 Arusha Wananchi wa jamii ya Wamaasai wilayani Ngorongoro, hususan Tarafa ya Sale, wameeleza wasiwasi wao kuhusu mapendekezo ya tume mbili za Rais zilizowasilishwa hivi karibuni, wakihofia huenda zisitoe suluhisho la changamoto zinazowakabili. Kupitia tamko lao la Machi 20, 2026, wananchi hao wanasema baada ya kuchambua ripoti hizo, wamebaini kuwa hazijaakisi kwa kina uhalisia wa maisha yao wala kuzingatia maoni waliyowasilisha wakati wa ukusanyaji wa taarifa. Wanasema kwa muda mrefu wamekuwa wakiishi ndani ya mfumo wa ikolojia wa Ngorongoro na Serengeti kwa kutegemea ufugaji, wakiamini kuwa mfumo huo umewezesha kuendelea kwa uhifadhi wa mazingira kwa vizazi vingi. Hata hivyo, wananchi hao wameeleza kuwa bado wanakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo upatikanaji wa maeneo ya malisho, ukamataji wa mifugo pamoja na vikwazo katika upatikanaji wa huduma za msingi. Aidha, wameeleza kuwa mapendekezo yanayohusu kuendelea kwa uhamishaji wa wananchi kutoka katika maeneo yao yameibua hof...

WANANCHI NGORONGORO WATAKA MAJIBU YA HARAKA KUHUSU RIPOTI ZA TUME ZA RAIS.

Image
  WANANCHI NGORONGORO WATAKA MAJIBU YA HARAKA KUHUSU RIPOTI ZA TUME ZA RAIS. ARUSHA Wananchi wa jamii ya Wamaasai katika Wilaya ya Ngorongoro wameeleza wasiwasi wao juu ya kucheleweshwa kwa ripoti za tume mbili za Rais zilizoundwa mwezi Februari mwaka 2025 kuchunguza migogoro ya ardhi katika eneo hilo. Kupitia taarifa kwa umma iliyotolewa Machi 5 mwaka huu, wananchi hao wamesema tume hizo zilipewa muda wa siku 90 kukamilisha kazi na kuwasilisha ripoti zake, ambapo zilitarajiwa kukamilika Mei 2025 lakini hadi sasa bado hazijatolewa. Wananchi hao wanasema kucheleweshwa kwa ripoti hizo kumeibua hofu na taharuki miongoni mwao, huku wakisubiri kwa hamu majibu ya masuala waliyowasilisha mbele ya tume hizo ikiwemo changamoto za matumizi ya ardhi, huduma za kijamii pamoja na mpango wa serikali wa kuwahamisha wakazi kutoka Hifadhi ya Ngorongoro kwenda kijiji cha Msomera mkoani Tanga. Aidha, wananchi hao wamedai kuwepo kwa vitendo vya kukamatwa kwa mifugo, kuvunjwa kwa nyumba na vikwazo vya ...
Image
  SERIKALI YAIMARISHA MIUNDOMBINU YA AFYA ARUSHA, YAAGIZA UJENZI WA GOROFA KITUO CHA AFYA KALOLENI. Serikali kupitia Wizara ya Afya imeendelea kuimarisha miundombinu ya utoaji wa huduma za afya nchini, ambapo Waziri wa Afya, Mohamed Mchengerwa, ameziagiza mamlaka za Halmashauri ya Jiji la Arusha kuanza mara moja ujenzi wa jengo la gorofa katika Kituo cha Afya Kaloleni ili kukabiliana na msongamano mkubwa wa wagonjwa. Waziri Mchengerwa ametoa maagizo hayo wakati wa ziara ya kikazi ya kukagua utoaji wa huduma za afya katika kituo hicho, akisema idadi kubwa ya wananchi wanaohitaji huduma imekuwa ikiongezeka, hali inayosababisha changamoto katika utoaji wa huduma kwa ufanisi. Amesema ujenzi wa jengo la gorofa utasaidia kuongeza wigo wa huduma, kuboresha mazingira ya kazi kwa wahudumu wa afya na kuhakikisha wananchi wanapata huduma kwa wakati na kwa ubora unaostahili. Katika hatua nyingine, Waziri Mchengerwa amesifu jitihada za watoa huduma wa afya katika Kituo cha Afya Kaloleni, akiwem...

SIKU 100 ZA RAIS SAMIA: KAMATI YA BUNGE YARIDHISHWA NA KASI YA WIZARA YA NISHATI.

Image
Na Mwandishi Wetu, Dodoma Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini imeipongeza Wizara ya Nishati kwa kazi kubwa inayoendelea kutekelezwa ndani ya siku 100 za uongozi wa Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ikiwemo kuanza kusambaza umeme katika vitongoji 9,009, hatua inayoonesha mwelekeo chanya wa utendaji wa kipindi cha pili cha Serikali ya Awamu ya Sita. Pongezi hizo zimetolewa Januari 20, 2026 jijini Dodoma na Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Mhe. Subira Mgalu, wakati wa kikao cha kwanza kati ya Wizara ya Nishati, taasisi zilizo chini yake pamoja na Kamati hiyo.  Kikao hicho kimelenga kuijengea Kamati uelewa kuhusu muundo na majukumu ya Wizara ya Nishati, pamoja na sera na sheria mbalimbali zinazosimamiwa na Wizara hiyo katika kuendeleza Sekta ya Nishati nchini. Akizungumza katika kikao hicho, Mhe. Mgalu amesema mafanikio yaliyopatikana ndani ya siku 100 za uongozi wa Rais Samia ni ushahidi wa dhamira ya Serikali katika kuhakikisha upatikanaji wa nishati ya uhakika kwa wananchi....

GHANA, TANZANIA STRENGTHEN LOCAL CONTENT COLLABORATION IN MINING.

Image
  📍Accra, Ghana Tanzania is set to deepen domestic participation, industrial growth and value retention in its mining sector following the strengthening of institutional collaboration with Ghana on Local Content implementation. The two countries are enhancing cooperation on policies and best practices aimed at increasing the participation of local citizens and firms across the mining value chain, strengthening domestic institutions and ensuring that a greater share of mineral wealth benefits national economies. This was underscored during an official experience-sharing visit by a delegation from Tanzania’s Mining Commission to Ghana’s Minerals Commission, which focused on exchanging knowledge, policy approaches and implementation frameworks for Local Content in the mining sector. Speaking during the visit, Chairperson of the Local Content Committee from Tanzania, Dr Theresia C. Numbi, said Local Content is not merely a legal requirement but a strategic tool for national developmen...

POLISI WAKANUSHA TAARIFA YA KUCHOMWA KWA NYUMBA YA ASKARI ARUSHA.

Image
  ARUSHA. Na Gladness Kowero.  Jeshi la Polisi Mkoa wa Arusha limekanusha taarifa inayosambaa katika mtandao wa kijamii ikieleza kuwa nyumba ya kiongozi wa Polisi Mkoani humo imechomwa moto. Akitoa taarifa hiyo leo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi SACP Justine Masejo amesema Jeshi hilo linaendelea kuwasiliana na mamlaka zinazosimamia vyombo vya habari na zile zinazo husika na ulinzi wa taarifa binafsi kwa hatua zaidi za kisheria. Aidha, ametoa wito na onyo kwa baadhi ya watu wenye tabia za kuandaa na kusambaza taarifa za uongo, kupandikiza chuki na kuchonganisha jamii kuacha kufanya hivyo kwani ni kinyume na sheria. Sambamba na hilo amebainisha kuwa watu wanaosambaza taarifa kama hizo hawanufaishi jamii na wala haziwanufaishi hata wao wenyewe.