SERIKALI YAIMARISHA MIUNDOMBINU YA AFYA ARUSHA, YAAGIZA UJENZI WA GOROFA KITUO CHA AFYA KALOLENI. Serikali kupitia Wizara ya Afya imeendelea kuimarisha miundombinu ya utoaji wa huduma za afya nchini, ambapo Waziri wa Afya, Mohamed Mchengerwa, ameziagiza mamlaka za Halmashauri ya Jiji la Arusha kuanza mara moja ujenzi wa jengo la gorofa katika Kituo cha Afya Kaloleni ili kukabiliana na msongamano mkubwa wa wagonjwa. Waziri Mchengerwa ametoa maagizo hayo wakati wa ziara ya kikazi ya kukagua utoaji wa huduma za afya katika kituo hicho, akisema idadi kubwa ya wananchi wanaohitaji huduma imekuwa ikiongezeka, hali inayosababisha changamoto katika utoaji wa huduma kwa ufanisi. Amesema ujenzi wa jengo la gorofa utasaidia kuongeza wigo wa huduma, kuboresha mazingira ya kazi kwa wahudumu wa afya na kuhakikisha wananchi wanapata huduma kwa wakati na kwa ubora unaostahili. Katika hatua nyingine, Waziri Mchengerwa amesifu jitihada za watoa huduma wa afya katika Kituo cha Afya Kaloleni, akiwem...