Posts

Showing posts from March, 2026

WANANCHI WA NGORONGORO WAIBUA WASIWASI KUHUSU MAPENDEKEZO YA TUME.

Image
 Arusha Wananchi wa jamii ya Wamaasai wilayani Ngorongoro, hususan Tarafa ya Sale, wameeleza wasiwasi wao kuhusu mapendekezo ya tume mbili za Rais zilizowasilishwa hivi karibuni, wakihofia huenda zisitoe suluhisho la changamoto zinazowakabili. Kupitia tamko lao la Machi 20, 2026, wananchi hao wanasema baada ya kuchambua ripoti hizo, wamebaini kuwa hazijaakisi kwa kina uhalisia wa maisha yao wala kuzingatia maoni waliyowasilisha wakati wa ukusanyaji wa taarifa. Wanasema kwa muda mrefu wamekuwa wakiishi ndani ya mfumo wa ikolojia wa Ngorongoro na Serengeti kwa kutegemea ufugaji, wakiamini kuwa mfumo huo umewezesha kuendelea kwa uhifadhi wa mazingira kwa vizazi vingi. Hata hivyo, wananchi hao wameeleza kuwa bado wanakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo upatikanaji wa maeneo ya malisho, ukamataji wa mifugo pamoja na vikwazo katika upatikanaji wa huduma za msingi. Aidha, wameeleza kuwa mapendekezo yanayohusu kuendelea kwa uhamishaji wa wananchi kutoka katika maeneo yao yameibua hof...

WANANCHI NGORONGORO WATAKA MAJIBU YA HARAKA KUHUSU RIPOTI ZA TUME ZA RAIS.

Image
  WANANCHI NGORONGORO WATAKA MAJIBU YA HARAKA KUHUSU RIPOTI ZA TUME ZA RAIS. ARUSHA Wananchi wa jamii ya Wamaasai katika Wilaya ya Ngorongoro wameeleza wasiwasi wao juu ya kucheleweshwa kwa ripoti za tume mbili za Rais zilizoundwa mwezi Februari mwaka 2025 kuchunguza migogoro ya ardhi katika eneo hilo. Kupitia taarifa kwa umma iliyotolewa Machi 5 mwaka huu, wananchi hao wamesema tume hizo zilipewa muda wa siku 90 kukamilisha kazi na kuwasilisha ripoti zake, ambapo zilitarajiwa kukamilika Mei 2025 lakini hadi sasa bado hazijatolewa. Wananchi hao wanasema kucheleweshwa kwa ripoti hizo kumeibua hofu na taharuki miongoni mwao, huku wakisubiri kwa hamu majibu ya masuala waliyowasilisha mbele ya tume hizo ikiwemo changamoto za matumizi ya ardhi, huduma za kijamii pamoja na mpango wa serikali wa kuwahamisha wakazi kutoka Hifadhi ya Ngorongoro kwenda kijiji cha Msomera mkoani Tanga. Aidha, wananchi hao wamedai kuwepo kwa vitendo vya kukamatwa kwa mifugo, kuvunjwa kwa nyumba na vikwazo vya ...